Adabu za Kusoma Qur’an

Download: Bonyeza nukta (dots) tatu kupata darsa kwa simu yako

Ni lazima kwa msomaji kujipamba na adabu za kisomo ambazo anatakiwa kujipamba nazo ikiwa ni pamoja na:

1 – Kumtakasia nia Allaah (Ta´ala).

2 – Kusoma akiwa na twahara.

3 – Kutumia Siwaak.

Kufanya mambo hayo ni katika kuyaadhimisha maneno ya Allaah (´Azza wa Jall).

4 – Ni lazima kwake kusoma kwa kutamka. Ambaye atatosha kusoma kwa kuangalia peke yake hazingatiwi kasoma na hapati thawabu za kisomo.

5 – Ni lazima kwake kuyazingatia yale anayoyasoma. Kwa sababu hayo ni miongoni mwa malengo yanayotakiwa.

6 – Miongoni mwa adabu za kisomo ni msomaji asujudu pale atapoipitia Aayah ya kisomo ilihali ametawadha pasi na kujali ni wakati gani.

7 – Asisome kwa sauti kwa njia ya kwamba akawakera walioko pambizoni mwake. Abu Sa´iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza:

“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliikaa I´tikaaf msikitini. Akawasikia wakisoma kwa sauti za juu akiwa kwenye hema lake akafunua pazia na kusema: “Zindukeni! Nyote ni wenye kumng´oneza Mola Wenu. Kwa hivyo baadhi wasiwaudhi wengine na baadhi yenu wasiwanyanyulie wengine kisomo” au alisema “… katika swalah.” [Abu Daawuud (1332), an-Nasaa´iy katika ”al-Kabiyr” (07/288, 289) na Ahmad (18/392-393). al-Albaaniy amesema: ”Cheni ya wapokezi wake ni Swahiyh juu ya sharti za al-Bukhaariy na Muslim.” Tazama ”as-Swahiyhah” (04/134).]

‘Subhanaka Allahumma wa bihamdika, ash-hadu an la ilaha illa Anta, astaghfiruka wa atubu ilaika 

(O Allah, You are free from every imperfection; praise be to You. I testify that there is no true god except You; I ask Your Pardon and turn to You in repentance)

Share this, BaarakAllah Feekum: [“One who guides to something good has a reward similar to that of its doer”] – Hadeeth

Mshirikishe mwenzako (Share)

The Most Comprehensive and Authentic Explaination of the Quran!
Tafsir Ibn Kahtir (10 Vol)
Purchase the complete Tafsir Ibn Kathir (10 Vol Abridged) By Dar-us-Salam Publications.